Inawezekana !!!!!

Jiamini unaweza na ufanye unachoamini!!

Saturday, January 28, 2012

Hohenzollernbruecke Bridge - The Bridge of Love


Thousands upon thousands of locked padlocks can be seen affixed to the fence across the unpronounceable Hohenzollernbruecke bridge in Cologne, Germany. The phenomenon called Love Locks (or Love Padlocks), which many believe to have originated from Italy, is a new kind of vandalism where lovebirds lock padlocks bearing their names against fences, gate, bridge or similar public place to symbolize their everlasting love.
According to Wikipedia, Love padlocks have existed for quite some time, though there are no certain sources for their origin. In Europe, love padlocks started appearing in the early 2000s. In Rome, the ritual of affixing love padlocks to the bridge Ponte Milvio can be attributed to the book I Want You by Italian author Federico Moccia, who later made it into the film-adaptation Ho voglia di te.

A similar bridge in Serbia exist, where the practice of love locks can be traced to before World War I. The story goes as that there was a local schoolmistress named Nada, from Vrnjacka Banja, who fell in love with a Serbian officer named Relja. After they committed to each other Relja went to war in Greece where he fell in love with a local woman from Corfu. As a consequence, Relja and Nada broke up their engagement. Nada never recovered from that devastating blow, and after some time she died as a result of her unfortunate love. As young girls from Vrnjacka Banja wanted to protect their own loves, they started writing down their names, together with the names of their loved ones, on padlocks and affixing them to the railings of the bridge where Nada and Relja used to meet.

Love Locks are frowned upon by the local authorities and owners of various landmarks. Some years ago, Deutsche Bahn, the Hohenzollernbruecke bridge operator, threatened to have the locks removed from the bridge but in the end relented in the face of public opposition.
Love locks are a growing phenomenon in cities across Europe. They have even appeared along the Wild Pacific Trail in Ucluelet on Vancouver Island in Canada.



Posted by Safari at Saturday, January 28, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 

For the Ladies awesome creative High Heels























Posted by Safari at Saturday, January 28, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 

Tuesday, January 24, 2012

PAC YATAKA SHERIA EWURA IBADILISHWE

KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma(PAC), imeagiza kwamba sheria inayoruhusu Mamlaka ya Nishati na Madini(EWURA) kulipa mishahara ya watumishi wa Baraza Ushauri na Watumaji la Nishati na Madini (EWURA CCC) ibadilishwe ili baraza hilo liweze kufanya kazi ipasavyo.

Hayo yalisemwa leo na Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe wakati akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye ofisi ndogo za Bunge jijini Dares Salaam kuhusu shughuli zilizofanywa na kamati yake , ambapo alisema baraza hilo hesabu zake zinakwenda vizuri.

“Baraza hili hesabu zake ni nzuri , lakini halifanyi kazi ipasavyo kwa kuwa halimtendei kazi ipasavyo liko pamoja na EWURA tumeagiza sheria ibadilishwe ili liweze kufanya kazi kwa kuzingatia pande zote,” alisema Filikunjombe.

Makamu Mwenyekiti huyo alishauri kuwa ni vyema mishahara hiyo ilipwe na wizara husika ili baraza hilo lifanye kazi bila kuegemea upande mmoja.

Akizungumzia kuhusu upandaji wa umeme kwa asilimia 40 alihojia upanda kwa sababu zipi je mlaji wa chini wamemsikiliza wanasemaje, hivyo alisema haitakuwa sahihi ikiwa hakusikilizwa.

Aliongeza kuwa baraza hilo pia linatakiwa kuacha kulipa malipo ya kila baada ya miaka mitano mtumishi anapostaafu badala yake yawe katika mfumo ya mifuko ya hifadhi ya jamii, ikiwemo kuwaingiza watumishi wake katika Mfuko wa Bima ya Afya ili kuepuka utumiaji wa risiti za malipo ya matibabu.

Alitaka baraza hilo kutumia fedha kulingana na bajeti yake.

Wakati huohuo Filikunjombe alisema kamati hiyo imemfukuza mwakilishi wa Shirika Hodhi la Mali za Umma (CHC) kwa kuwa ni mtendaji wa chini hawawezi kuzungumza naye hivyo wanamtaka Ofisa Mtendaji Mkuu.

Alisema mwakilishi aliyetumwa ni Ofisa Uhusiano ambayo ameitumwa na Kaimu Mkurugenzi.
Posted by Safari at Tuesday, January 24, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AANZA ZIARA YA MKOA WA TANGA LEO, AKAGUA UKUTA WA KUZUIA MAJI YA BAHARI PANGANI

Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi Jengo la Ofisi ya Idara ya Maji, lililopo Wilaya ya Pangani, wakati alipoanza ziara yake ya Mkoa wa Tanga leo, Januari 24, 2012. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa (kushoto) ni Mkurugenzi wa Maji wa wilaya hiyo, Mohamed Hamis. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kuhusu ukuta huo unaozuia maji ya Bahari unaobomoka kutokana na mabadiliko ya Tabia nchi na kutishia amani ya wakazi wa maeneo hayo. Pangani Kivukoni. Picha na Muhidin Sufiani-OMR Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na baadhi ya Viongozi wa Wilaya ya Pangani wakati akitoka kukagua ukuta wa kuzuia maji ya Bahari unaobomoka Pangani Kivukoni. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia ukuta unaozuia maji ya Bahari eneo la Pangani Kivukoni, unaozidi kubomoka kutokana na kujengwa miaka 100 iliyopita na kutishia amani kwa wakazi wa maeneo hayo. Makamu wa Rais ameanza ziara yake ya Mkoa wa Tanga leo Januari 24, 2012. Picha na Muhidin Sufiani-OMR
Posted by Safari at Tuesday, January 24, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 

Saturday, January 21, 2012

kipindi cha kijamii cha weekend specila cha wapo redio fm chatimiza miaka 5

Baada ya shughuli nzima ya maadhimisho ya miaka 5 ya kipindi cha Weekend Special,kinachorusha na redio ya Wapo FM,wageni waalikwa walipata picha ya pamoja kama ukumbusho muhimu kwao,nje ya jengo la mikutano la Taasisi ya Maendeleo ya Vijana (UVIKIUTA),iliopo Chamazi-Mbagala jijini Dar.

Keki tuliii safi kabisa.

Mmoja wa wageni kutoka meza kuu,Wakili wa Kujitegemea Bw. Emanuel Makene akikata keki kwa ajili ya kulishwa wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye maadhimisho ya kipindi hicho ambacho kimekuwa kikipendwa na kusikilizwa sana wanajamii.

Mtangazaji wa Wapo FM,Dada Benedict Mrema akichombeza hapa na pale,huku muasisi wa kipindi cha Weekend Special,Antony Joseph akitaka kuwalisha wageni waalikwa keki iliondaliwa maalum kwa maadhimisho ya miaka 5 ya kipindi hicho tangu kuanzishwa kwake.

Keki ikigaiwa kwa wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo.

Mmoja wa wasanii kutoka Taasisi ya Maendele ya Vijana (UVIKIUTA) akiwaburudisha wageni waalikwa

Mmoja wa vijana wajasiliamali akifafanua kuhusiana na matatizo mbalimbali wanavyokumbana nayo katika shughuli zao mbalimbali za kila siku za ujasiliamali.

Mtangazaji wa Wapo FM redip,Dada Ritha Chaula akisoma hotuba fupi kuhusiana na maadhimisho ya miaka 5 ya kipindi cha Weekend Special,mbele ya meza kuu na wageni waalikwa mbalimbali waliofika.kipindi hicho hurushwa kila siku ya jumamosi kuanzia saa 8 mchana mpaka 11.30 jioni kikiwa na lengo la kuelimisha,na kuipasha jamii maovu yanayotendeka,namna ya kukabiliana nayo na kuyaepuka,sambamba na hayo kipindi hicho pia huibua na kutangaza matukio ya unyanyapaa,unyanyasaji wa kijinsia,ubakaji na ulawiti,kuwapa vijana elimu ya stadi ya maisha ili waweze kujitambu,kujiamini na kujiajiri katika kuyakabili maisha kiuchumi,kuibua migogoro ya ndoa,kupata elimu ya namna ya kutatua na kupata suluhisho la kudumu.



Wadau wakifautilia kongamano wakati likiendelea.
Baadhi ya Watangazaji wa Wapo Fm redio wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokuwa yakijiri ndani ya ukumbi,wakati kongamano la vijana likiendelea.Sho ni DadaRitha Chiwalo,Benedict Mrema na mdau wa Wapo FM.

Pichani kulia ni Dada Faines Mwakatobe kutoka Chuo Kikuu Huria cha jijini Dar akiwatafsiria baadhi ya Walemavu wa kutosikia,ambao pia wameshiriki katika Maadhimisho ya miaka mitano (5) ya kipindi cha Weekend Special kinachorushwa na redio Wapo FM, kila siku ya jumamosi.Maadhimisho hayo yalikwenda sambamba na kongamano la vijana ambalo lilijadili changamoto mbalimbali zinazowakumba vijana katika nyanja mbalimbali kama vile uchumi,ajira,elimu na mambo mengineyo.

Baadhi ya wadau wa kipindi cha Njia Panda cha Clouds FM ambao pia wameshiriki katika Maadhimisho ya miaka 5 ya kipindi cha Weekend Special kinachorushwa na redio Wapo FM cha jijini Dar, kila siku ya jumamosi.

Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia kwa makini mijadala iliyokuwa ikitolewa kwenye maadhimisho hayo yaliyofana kwa kiasi kikubwa.

Waimbaji wa muziki wa nyimbo za Injili kutoka kundi la Double E likitumbuiza katika maadhimisho hayo.

Mtangazaji wa kipindi cha Wikend Special kinachorushwa na redio ya Wapo FM, ambacho leo kinaadhimisha miaka 5 tangu kuanzishwa kwake, Bw. Antony (kulia), akiwatambulisha viongozi wa vikundi mbalimbali mbele ya wageni waalikwa (hawapo pichani) waliofika kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyika leo kwenye viunga vya UVIKIUTA-Chamazi jijini.

Mwakilishi kutoka TYC, Bw. Nyakia Ally akizungumza machache mbele ya wageni waalikwa (ambao kwa asilimia kubwa ni vijana kutoka sehemu mbalimbali waliofika kwenye maadhimisho ya miaka 5 ya kipindi cha Special Wikend kinachorushwa na redio ya Wapo FM, anayefuata ni Wakili wa Kujitegemea Bw. Emanuel Makene, Dr. Nassoro Ally Matuzya kutoka hospitali ya Mwanyanyamala, Mmoja wa wakilishi kutoka chuo kikuu UDSM, Bw. Edward Daniel na shoto ni Mwendesha kipindi cha Wikend Special Bw.Antony Joseph.

Kongamano likiendelea kwa umakini kabisa.

Mmoja wa wanaharakati vijana,Dr Nassoro Ally Matuzya kutoka hospitali ya Mwanyanyamala akifafanua jambo ikiwa ni sehemu ya kongamano la vijana la kuelimishana kuhusiana na mambo mbalimbali zikiwemo changamoto wanazokabiliana/kumbana nazo katika mfumo mzima wa maisha yao ya kila siku.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili,Pius Senyagwa sambamba na wasanii wengine wakitumbuiza mbele ya wageni waalikwa kwenye maadhimisho hayo yaliyofana kwa kiasi kikubwa.

Makofi ya hapa na pale yalikuwepo kutoka kwa wageni waalikwa.

Baadhi ya vijana walioko kwenye Taasisi ya Maendeleo ya Vijana (UVIKIUTA),kutoka Mataifa mbalimbali wakifuatilia mijadala mbalimbali iliokuwa ikizungumzwa kwenye kongamano lililoendana sambamba na maadhimisho ya miaka 5 ya kipindi cha Weekend Special kinachorushwa na redio ya Wapo FM,jijini Dar,maadhimisho hayo yamefanyika kwenye viunga vya taasisi hiyo huko Chamazi-Mbagala jijini Dar.
Posted by Safari at Saturday, January 21, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 

WATEJA WA M-PESA WENYE AKAUNTI CRDB SASA KUWEKA NA KUTOA FEDHA KUPITIA SIMU YA MKONONI.




Wateja wa Vodacom M-PESA wenye akaunti katika benki ya CRDB sasa wanauwezo wa kuweka na kutoa fedha kutoka katika akaunti zao kupitia simu ya mkononi ya Vodacom iliyosajiliwa na huduma ya M-PESA.

Kuzinduliwa kwa huduma hiyo sasa kunawapa urahisi zaidi wateja wa Vodacom M-PESA kuweka na kuchukua fedha zao kutoka akaunti ya benki kwa urahisi na unafuu zaidi mahali popote nchini na kwa wakati wowote pasi na kulazimika kufika katika tawi la benki ya CRDB..

Huduma hii ya ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na kampuni ya Vodacom kupitia huduma yake ya M-PESA ni ya kwanza nchini na inalenga kuwaondolea usumbufu wateja wa M-PESA wa kupanga foleni ama kutembea umbali mrefu kufuata tawi la Benki.

“Tunapoitambulisha huduma hii mpya inaamaanisha kwamba tumeongeza thamani nyengine katika simu ya mkononi na huduma ya Vodacom M-PESA.Mteja wa M-PESA kuweza kutoa na kuchukua fedha kutoka akaunti zao za CRDB kupitia simu zao za mkononi ni hatua nyengine muhimu ya kujivunia kuwa mteja wa Vodacom”Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Bw. Rene Meza.

Huduma ya Vodacom M-PESA ya kwanza sokoni kutoka Vodacom mtandando unaoongoza nchini ni kielelezo makini cha ubunifu na namna ambavyo Vodacom imedhamiria kubadili maisha ya watu kupitia teknolojia ya simu za mkononi.

Ikiwa na mawakala zaidi 20,000 nchi nzima M-PESA inabakia kuwa huduma salama zaidi, ya haraka, uhakika na yenye kuaminika kwa ajli ya kuweka na kutuma fedha, kufanya malipo ya huduma na manunuzi mbalimbali, kulipia kodi, kuchangia pensheni pamoja na kupokea fedha kutoka nchi zaidi ya sabini na tano ulimwenguni.

“Hakuna mteja wa Vodacom M-pesa atakaesimama kwenye foleni au kulazimika kutembea umbali mrefu kufuata tawi la benki yake ya CRDB, sasa wataweka na kutoa fedha wakati wowte na mahali popote bila kuathiri shughuli nyengine za kijamii na kimaendeleo ni wazi maisha yamekuwa rahisi zaidi.”Aliongeza Bw. Rene

Tangu ilipoanzishwa mwaka 2007, huduma ya Vodacom M-PESA imeendelea kujipatia umaarufu mkubwa kutokana na kuwa huduma yenye usalam zaidi, yenye mtandao mpana wa mawakala mijini na vijijini na hivyo kuchangia maendeleo ya jamii na biashara nchini kwa kuinua vipato vya wananachi kupitia ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja.

Kuweka fedha katika akaunti ya CRDB kutoka akaunti ya M-PESA,hatua ni kama ifuatavyo

I. Piga *150#
II. Chagua kulipia bili
III. Ingiza namabri ya biashara ambayo ni 900500
IV. Ingiza nambari ya kumbukumbu ambayo ni namabri ya akaunti ya benki.
V. Weka kiasi cha fedha mteja anachotaka kutoa katika akaunti ya M-PESA kwenda akaunti ya benki
VI. Ingiza nambari ya siri.
VII. Bonyeza 1 kuthibitisha au 2 kubatilisha muamala.

Baada ya hatua hizi mteja atapokea mara moja ujumbe mfupi wa maneno – SMS kutoka M-PESA kuthibitisha muamala na baada ya dakika 8 atapokea ujumbe kutoka benki ya CRDB.

Kuhamisha fedha kutoka akaunti ya Benki ya CRDB kwenda M-PESA hatua ni kama ifuatavyo

I. Piga *150*03#
II. Ingzia nambari ya siri
III. Chagua nambari 3 (Hamisha fedha)
IV. Chagua nambari 3 (M-PESA)
V. Chagua nambari ya akaunti yako ya Benki
VI. Thibitisha nambari yako ya simu
VII. Ingiza kiasi cha fedha unachotaka kuhamisha
VIII. Thibitisha au batilisha. Na baada ya hapo utapokea ujumbe mfupi wa maneno – SMS kutoka M-PESA na pia Benki ya CRDB unaothibitisha zoezi hili.

Ili kuwa na uwezo wa kuhamisha fedha kutoka Benki kwenda M-PESA ni LAZIMA kwanza mteja wa M-PESA ajisajili CRDB.

Usajili huo hufanyika MARA MOJA TU na kwamba unaweza kufanyika kupitia simu ya mkononi kwa kupiga *150*03# na maelezo ya namna ya kujisajili yatatotekea ambayo mteja atapaswa kuyafuata.
Posted by Safari at Saturday, January 21, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 

Serikali yasema iko tayari kukutana na madaktari


Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Lucy Nkya

Siku chache baada ya Chama cha Madaktari nchini (MAT) kutangaza mgogoro na serikali na kuipa saa 72, serikali imetangaza kuwa ipo tayari kukaa nao meza moja na kuzungumzia masuala ya sekta ya afya.

Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Lucy Nkya, alitoa kauli hiyo jana na kusema kuwa serikali ipo tayari kukaa na MAT kuzungumza kama watakuwa tayari.

Dk. Nkya alisema sakata la madaktari 1,994 waliokuwa katika mazoezi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili waliamua kutoendelea na ratiba zao za mazoezi kwa vitendo baada ya kucheleweshewa posho zao za kila mwezi.

Alisema baada ya kuchelewa kutolewa kwa fedha za posho, wizara ilifanya jitihada ya kuhakikisha fedha hizo zinapatikana haraka.

Alisema serikali ilikuwa ikitoa taarifa katika taasisi walizokuwa wakifanyia kazi kuhusiana na jitihada zinazofanywa ili kutatua tatizo hilo.

“Ieleweke kwamba wataalamu hawa huingia mikataba na hospitali husika na mkataba wanaoingia umeainisha hawatakiwi kugoma au kuanzisha mgomo,” alisema Dk. Nkya.

Dk. Nkya alisema pamoja na wizara kufanya jitihada hizo kuwa suala lao limefanyiwa ufumbuzi, lakini bado walishikilia msimamo wao wa kutorudi vituoni hadi wapokee fedha na kwamba jambo hilo halikuwa la kiungwana.

Alisema baada ya kuona hivyo, wizara ilipeleka wataalamu 51 waliokuwa wakisubiri kuanza mafunzo Januari mwaka huu ili kuchukua nafasi za wataalamu waliokataa kurejea katika hospitali hiyo kwa ajili ya kuzuia athari ambazo zingeweza kujitokeza kwa wagonjwa. Hata hivyo, alisema katika mgomo huo kuna wenzao 60 ambao hawakugoma.

“Baadhi ya wataalamu waliokuwa wakifanya mazoezi katika vituo kama vya Hospitali ya KCMC, Mount Meru, Bombo, Bugando na Manispaa za Dar es Salaam walitambua jitihada za wizara za kushughulikia tatizo hilo na waliendelea na ratiba yao ya mazoezi kwa vitendo,” alisema.

Alisema waliogoma uongozi wa Muhimbili uliwachukulia hatua na kuwaandikia barua kuwarudisha wizarani na kutaka wapatiwe wataalamu hao.

“Ili kuhakikisha wataalamu hao wanafikia malengo ya mazoezi ya vitendo wizara imeamua kuwapanga katika hospitali mbalimbali ikiwemo Muhimbili, Temeke, Mwananyamala, Aga khan, Amana na Lugalo kwa kuzingatia uwezo wa hospitali,” alisema.

Alisema Januari 16, mwaka huu wataalamu 194 walikuwa wamepewa barua na wameripoti katika vituo walivyopangiwa.

Alisa wizara yake imepata taarifa kupitia vyombo vya habari kuwa MAT imewapa saa 72 iwarudishe madakatari hao katika hospitali ya Muhimbili pamoja na kutaka kuondolewa kwa baadhi ya viongozi wa wizara.

Hata hivyo, alisema tamko hilo halijawasilishwa rasmi wizarani na kusisitiza kuwa madakatari hao hawajafukuzwa kufanya mazoezi bali wamepangiwa vituo vingine.

Akizungumzia uamuzi wa MAT kumvua uanachama Mganga Mkuu wa Serikali, Deo Mtasiwa, Dk. Nkya alisema chama hicho hakiwezi kumchukulia hatua bali chombo chenye mamlaka ni Wizara.

Rais wa MAT, Dk. Namala Mkopi, alisema suala hilo watalizungumzia leo na kwamba tamko walilolitoa Jumamosi sio lazime lipelekwe wizarani ndio maana walitoa taarifa kupitia vyombo vya habari.

CHANZO: NIPASHE
Posted by Safari at Saturday, January 21, 2012 0 comments Links to this post
Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to Facebook
Reactions: 
Older Posts Home
Subscribe to: Posts (Atom)

Matangazo

yanahitajika kwa bei nafuu tutakurushia hapa.

East African Time

Safari Dennis.

Maoni/Salamu !!


zKaribuni sana kwa kuangalia na Maoni.

Haya jamani msisite kutuma maoni na maswala yoyote yanayohusu jamii kwa kutumia mail yangu safari2tz@gmail.com

Kwa ajili ya kuangalia site nyingine !!

  • CULINARY CHAMBER
  • www.hisapepe.com/pages/index.php?refid=kadidi2
  • www.mactemba.blogspot.com
  • www.mazingirachanya.blogspot.com
  • www.zachariahtz.blogspot.com

Blog Mnaionaje ?

Total Pageviews

Load Counter
obagi

Followers

Kutafuta site mbali mbali

Loading...

Karibu ujionee Tanzania yetu na Dunia kwa ujumla.

Endelea

Habari zilizopo.

  • ▼  2012 (14)
    • ▼  January (14)
      • Hohenzollernbruecke Bridge - The Bridge of Love ...
      • For the Ladies awesome creative High Heels
      • PAC YATAKA SHERIA EWURA IBADILISHWE KAMATI ...
      • MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AANZA ZIARA YA MKOA WA ...
      • kipindi cha kijamii cha weekend specila cha wapo ...
      • WATEJA WA M-PESA WENYE AKAUNTI CRDB SASA KUWEKA N...
      • Serikali yasema iko tayari kukutana na madaktari ...
      • AJIRA MPYA ZA WALIMU ZATANGAZWA MAJINA YATOLEWA ...
      • MREMBO AUWAWA NIGERIA KISA FACEBOOK UHUSI...
      • Iran yataka mazungumzo na Marekani bila masharti ...
      • Ni safari ya Regia Mtema Maafisa Usalam...
      • Majambazi wavamia ndege ya dhahabuSubmitted by Mje...
      • Tiger Woods’ ex-wife bulldozes $12 million homeCou...
      • Happy New Year Happy New Year guys.Wishing you a...
  • ►  2011 (178)
    • ►  December (4)
      • MATUNDA YA LEMA YAANZA KUONEKANA WORLD BANK WAHOJI...
      • TAARIFA YA TAHADHARI.
      • New Joint: Ndoa ndoano by Kassim Mganga feat Mr Bl...
      • HABARI NJEMA SANA KWA WANAWAKE NA WANAUME WENYE MA...
    • ►  September (1)
      • 5 Foods That Can Trigger a Stroke
    • ►  July (4)
      • True Story. TRUE TO LIFE !!!!!!!!!!!!!! A w...
      • How 2 Keep Your GirlFriend Happy..... 1 - Dont...
      • 9 things you shouldn’t say to your childBy Sara Co...
      • This is really a new perspective about a boyI thin...
    • ►  June (12)
      • Awesome Breathing Therapy For Everyone Breathing T...
      • ALLY KIBA KAPATA AJALI MIKUMI MOROGORO Haba...
      • Quotable Quotes Napoleon said.. "The world suffe...
      • Delicious Fruits 01. Strawberries Strawber...
      • <!--[if gte mso 9]> Normal 0 f...
      • How to travel Safe With Girls Seat Belt The...
      • ...
      • Heart Attacks And Drinking Warm Water very goo...
      • Dead lock Boss said to secretary: For a week we ...
      • Du unaona Vyeo Hivyo !! Mie kuna mdau mmoja niliw...
      • <!--[if gte mso 9]> Normal 0 f...
      • Mnasubiria bajeti ya kuwaletea maisha bora? Mzee ...
    • ►  May (25)
      • <!--[if gte mso 9]> Normal 0 f...
      • <!--[if gte mso 9]> Normal 0 f...
      • GOLDEN GEMS OF THE WEEKÂ ...
      • Candle never looses its light- Good Morning
      • Husband and wife saga.. goes on and on...
      • How To Get Fit Being At Home
      • Dr. Oz's 100 Weight Loss Tips | The Dr. O...
      • Exams are like Girl friends ...
      • Contrary Proverbs Read and enjoy the fol...
      • God is like anti-...
      • Health Six Foods To Keep You Young
      • <!--[if gte mso 9]> Normal 0 f...
      • MAAJABU YA MAJI Na mwandishi Mrisho Abdall...
      • MAAJABU YA NDIZI MBIVU Ni kinga dhidi ya ma...
      • <!--[if !mso]> v\:* {behavior:url(#default#VML);}...
    • ►  April (36)
    • ►  March (18)
    • ►  February (16)
    • ►  January (62)
  • ►  2010 (384)
    • ►  December (28)
    • ►  November (11)
    • ►  October (21)
    • ►  September (33)
    • ►  August (34)
    • ►  July (34)
    • ►  June (43)
    • ►  May (17)
    • ►  April (16)
    • ►  March (73)
    • ►  February (61)
    • ►  January (13)
  • ►  2009 (527)
    • ►  December (63)
    • ►  November (13)
    • ►  October (16)
    • ►  September (82)
    • ►  August (34)
    • ►  July (80)
    • ►  June (37)
    • ►  May (58)
    • ►  April (19)
    • ►  March (67)
    • ►  February (28)
    • ►  January (30)
  • ►  2008 (2137)
    • ►  December (127)
    • ►  November (80)
    • ►  October (217)
    • ►  September (229)
    • ►  August (293)
    • ►  July (363)
    • ►  June (290)
    • ►  May (172)
    • ►  April (222)
    • ►  March (144)
Awesome Inc. template. Template images by mammamaart. Powered by Blogger.